Saturday, March 17, 2012


KONGAMANO LA KITAIFA LA USAFIRI WA ANGA (NATIONAL AIR TRANSPORT FORUM) TAREHE 21-22 MACHI 2012





Wizara ya Uchukuzi kwa kushirikiana na Sekta binafsi imeandaa Kongamano la Taifa la Usafiri wa Anga litakalofanyika Dar es Salaam kwenye Hoteli ya Serena zamani Movenpick kuanzia tarehe 21 - 22 Machi, 2012.

Kongamano hili litajadili maendeleo ya Usafiri wa Anga hapa nchini, changamoto zinazokabili sekta ya anga na namna ya kubaliana nazo. Aidha,  washiriki pia watajadili kwa kina mchango unaoweza kutolewa na usafiri wa Anga katika  ukuaji wa pato la Taifa.

Washiriki wa Kongamano hili ni wadau kutoka sekta ya usafiri wa anga wa ndani na nje ya nchi pamoja na sekta nyingine kama vile Fedha, Nishati na Madini, Mawasiliano, Uchukuzi, hali ya Hewa na nyinginezo.

Kongamamo hilo litaanza saa 3.00 asubuhi

Kwa taarifa zaidi tembelea tovuti ifuatayo: http://www.newhorizonstz.com

No comments:

Post a Comment