Tuesday, May 1, 2012

Wizara ya Uchukuzi siku ya Ijumaa tarehe 27 Aprili 2012 ilizindua rasmi Baraza lake la Wafanyakazi. Uzinduzi wake ulifanyika Mkoani Tanga katika Hoteli ya Mkonge na Waziri wa Uchukuzi Mhe Omari R. Nundu(Mb).



Wajumbe wa Baraza la wafanyakazi Bibi J. Ndaba, Bw. E. Mkiaru(mwenye suti nyeusi), Bw L. Lwiza (mwenye tai nyeusi) na Bibi J. Akile (aliyevaa kitenge) wakijadiliana jambo wakati wakisubiri ujio wa Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi ambaye ni Katibu Mkuu Mhandisi Omar A. Chambo.


Mjumbe Bw. T. Kasambala(mwenye shati jekundu) akibadilishana mawazo na na mjumbe mwenzie Bw. B.Chiganga(aliyesimama)kabla ya kuwasili kwa Mwenyekiti wa Baraza Mhandisi Omar A. Chambo.


Wajumbe wa Baraza Bi. A. Selemani(mwenye ushungi) na Bw. Ndumbaro(mwenye suti nyeusi) wakiteta jambo kabla ya kuanza kikao cha Baraza.


Wajumbe wakipitia vitabu vyenye taarifa za kikao kabla ya uzinduzi wa Baraza.



Wajumbe Bw. E. Mgawe(wa kwanza kushoto), Bw Manongi(wa pili kushoto), Bw N. Kirenga(wa pili toka kulia) na Dkt. ...(wa kwanza kulia)wakibadilishana mawazo kabla ya uzinduzi wa Baraza.








Wajumbe wakibadilishana mawazo na kupitia makabrasha kabla ya kuanza kwa kikao cha baraza.




Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu(DAHRM) Bibi J. Ndaba akimkaribisha Mwenyekiti wa Baraza Mhandisi Omar A. Chambo(aliyekaa katikati) kabla ya kufungua kikao cha baraza. Kushoto kwa Mwenyekiti katika picha ni Bw.Matiku - Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi(TUGHE) Wizarani, Mwakilishi wa Chama cha Wafanyakazi Mkoa(mwenye kofia) na Mwezeshaji toka Wizara ya Kazi na Ajira(mwenye suti ya kijivu).


Kamati ya Uchaguzi ikihesabu kura za majina yaliyopendekezwa kuongoza baraza yaani Katibu na Naibu Katibu ambapo Bw. Hassan Mabula alichaguliwa kuwa Katibu na Bibi Ruth Kigera alichaguliwa kuwa Naibu Katibu.


Mwenyekiti wa Baraza na Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Mhandisi Omar A. Chambo(wa kwanza kulia), Kaimu Mkurugenzi  wa Huduma za Uchukuzi Mhandisi Saad Fungafunga(katikati) na Katibu wa Baraza Bw. Hassan Mabula(kushoto) wakimsubiri Waziri wa Uchukuzi Mhe. Omari R. Nundu kabla ya uzinduzi wa Baraza.



Mwenyekiti wa Baraza Mhandisi Omar A. Chambo pamoja na Wakuu wa Taasisi na Idara/Vitengo wakimsubiri Waziri wa Uchukuzi Mhe.Omari R. Nundu.


Waziri wa Uchukuzi Mhe. Omari R. Nundu(Mb) akisalimiana/akipokewa na Mkurugenzi wa Huduma za Uchukuzi Mhandisi S. Fungafunga kabla uzinduzi wa Baraza. Wengine katika picha ni Mwenyekiti wa Baraza Mhandisi Omar A. Chambo pamoja na Wakuu wa Idara na Taasisi zilizo chini ya Wizara.



Waziri wa Uchukuzi Mhe. Omari R. Nundu akijadiliana jambo na Mwenyekiti wa Baraza Mhandisi Omar A. Chambo pamoja na Wakuu wa Idara na Taasisi zilizo chini ya Wizara kabla ya kuzindua Baraza.










Waziri wa Uchukuzi Mhe. Omari R. Nundu akisalimiana na Wakuu wa Taasisi na Idara wakati akiingia katika Ukumbi wa Mkutano wa Hoteli ya Mkonge kuzindua Baraza.


Baadhi ya wajumbe wa Baraza(kutoka kushoto) Bw Butallah, Bw. Chande na Bw. Mangosongo wakimkaribisha ukumbini Waziri wa Uchukuzi Mhe. Omari R. Nundu(hayupo pichani).