Tuesday, December 27, 2011

TAARIFA KWA UMMA NA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU RELI YA KATI
Kutokana na Mvua kubwa zinazonyesha maeneo mbalimbali ya reli ya Kati, Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) umeamua kuchukua uamuzi wa kufuta safari zote za Treni za abiria kutoka Dar es Salaam kwenda Kigoma kuanzia leo Jumanne Desemba 27, 2011 hadi itakavyotangazwa vinginevyo.

Kwa hiyo basi abiria wote waliokuwa wamepanga kusafiri leo na pia katika treni zijazo wanatakiwa kufika na tiketi zao katika ofisi za Stesheni Masta husika ili warejeshewe fedha za nauli walizolipa.

Tafadhali atakayesoma habari hii awaarifu na wengine.

Uongozi wa TRL unasikitika kwa usumbufu wote uliojitokeza.

Imetolewa na Ofisi ya Uhusiano -TRL


No comments:

Post a Comment