Saturday, December 3, 2011

Rais wa Zanzibar afungua Rasmi maonesho ya Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara - Viwanja vya JK Nyerere (Viwanja vya Sabasaba)


Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Mhandisi Omar A. Chambo (wa kwanza kushoto) akiwa pamoja na viongozi wengine wa Serikali pamoja na wananchi na wadau mbalimbali wakisubiri ujio wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein katika viwanja vya Julius Kambarage Nyerere.




Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Mhandisi Omar A. Chambo akiteta jambo wakati wakisubiri ujio wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk Ali Mohamed Shein.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein (wa tatu kutoka kushoto), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwezeshaji na Uwekezaji Dk Mary Nagu (wa pili kutoka kushoto), Katibu Mkuu Kiongozi Philemon Luhanjo (wa kwanza kulia), viongozi wengine wa Serikali na wadau mbalimbali wakiimba wimbo wa Taifa mara baada ya Rais kuwasili.




 Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Mhandisi Omar A. Chambo (wa pili toka kulia) pamoja voingozi wengine wa Serikali wakiangalia ngoma za asili wakati wa ufunguzi wa maonesho ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara.


Katibu Mkuu Kiongozi na Mwenyekiti wa Kamati ya Maadhimisho na Sherehe za Taifa Philemon Luhanjo akiwakaribisha Mgeni wa Heshima, viongozi wa Serikali na wageni wengine waalikwa.


Mgeni rasmi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein pamoja na viongozi wengine wakisikiliza hotuba ya ukaribisho ya Mwenyekiti wa Kamati ya Maadhimisho na Sherehe za Taifa Philemon Luhanjo.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwezeshaji na Uwekezaji Dk Mary Nagu akielezea manufaa ya maonesho ya maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru wa Tanzania Bara huku Mgeni Rasmi na viongozi wengine wa Serikali wakimsikiliza.

Mgeni Rasmi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk Ali Mohamed Shein akihutubia viongozi wa serikali, wageni waalikwa, wananchi na wadau mbalimbali waliohudhuria sherehe za ufunguzi wa maonesho. Wengine katika picha wakimsikiliza mgeni rasmi ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwezeshaji na Uwekezaji Dk Mary Nagu(mwenye kofia nyekundu).

No comments:

Post a Comment